Afisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa Hakimiliki Doreen Anthony Sinare akizungumza umuhimu wa kuhuwisha utafiti wa mchango wa Hakimiliki katika Pato la Taifa uliofanyika 2009-2010 kwa ufadhili wa Shirika la Miliki Bunifu Duniani (WIPO) katika kikao chake na Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt.Albina Chuwa kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu kilichofanyika Disemba 05,2023 Jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Ndg. Gerson Msigwa (aliyeketi katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa wa Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) mara baada ziara yake katika Ofisi hiyo Jijini Dar es Salaam Oktoba 31, 2023, wapili kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa Hakimiliki Doreen Anthony Sinare na wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.Dkt. Emmanuel Ishengoma.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Damas Ndumbaro atembelea Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA) Jijini Dar es Salaam Okoba 10,2023 ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kutembelea taasisi zilizochini ya Wizara yake kwa lengo la kufahamu majukumu .
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Ndg. Gerson Msigwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam Septemba 27, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Mhe. Dkt. Damas Daniel Ndumbaro kuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo katika hafla iliyofanyika Ikulu ndogo Tunguu Zanzibar tarehe 01 Septemba, 2023.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (aliyeketi katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Ofisi ya Hakimiliki Tanzania Bw. Victor Tesha (aliyesimama watatu kushoto) na pamoja na wajumbe wenzake mara baada ya uzinduzi wa Bodi hiyo, uliyofanyika Septemba 12, 2023 Jijini Dar es Salaamu .
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akimkabidhi Cheti cha Utambulisho wa Ubalozi wa Ofisi ya Hakimiliki Tanzania Msanii Barnaba Classic katika hafla ya Uzinduzi wa Bodi ya COSOTA na Bodi ya Bodi Filamu Septemba 12, 2023 Jijini Dar es Salaam.
Viongozi wa Taasisi zinazosimamia Miliki bunifu nchini COSOTA, BRELA, BPRA na COSOZA wakisaini makubaliano ya pamoja ya kuanzisha kituo cha kutoa elimu ya miliki bunifu nchini kwa kushirikiana na Shirika la Miliki bunifu Duniani (WIPO) katika hafla ya mgao wa mirabaha, pamoja na utoaji leseni kwa kampuni ya kukusanya na kugawa mirabaha kwa kazi za Muziki kufuatia mabadiliko ya Sheria ya Hakimiliki ya mwaka 2022 yaliyoliondolea COSOTA jukumu la kukusanya na kugawa mirabaha na kuwaruhusu wabunifu wenyewe kufanya hilo, Julai 21, 2023 Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Haraza Chana akikabidhi hundi ya mfano ya mgao wa mirabaha kwa bendi ya Msondo ngoma katika hafla ya mgao wa mirabaha Julai 21 , 2023 Jijini Dar es Salaam.